Maoni Ya Mwana-Buhigwe Na Ustawi Wa Kigoma

Pongezi nyingi, Mhe. Dr. Philip Mpango, kwa hatua ya kupewa nafasi kugombea uongozi, ngazi ya Ubunge, kwa ajili ya jimbo letu la Buhigwe, kupitia chama tawala. Mpaka hatua hii inapendeza kwamba umeaminiwa na wengi na kuonekana unafaa kuwaongoza wana-Buhigwe, na zaidi sana kuwawakilisha hatimaye katika Bunge la Jamhuri wa Muungano wa Tanzania – Mungu akipenda.